Jumapili, 16 Machi 2014

TUTHAMINI UTALII WA NDANI

Tanzania ni Nchi nzuri sana na ya kupendeza hayo ni maneno yanayoweza kumtoka mtu yeyote anayejua na kuelewa nini utalii, faida zake, umuhimu wake katika  jamii na hasa kwa wazawa, namaanisha Watu wa asili ya Tanzania (MTANZANIA)


Takwimu kupitia wizara husika inayohusiana na maswala ya utalii inaonyesha idadi ndogo sana ya watanzania wanaotembelea mbuga za wanyama na hata sehemu zingine za utalii hapa nchini  tofauti na wageni watokao Nchi za mbali  hasa Ulaya (Uingereza,Ujeruman Ubeligiji)  Marekani, China na nchi nyingine kote Duniani.

Utafiti uliofanyika unaonyesha sababu zifuatazo  ni chanzo cha wananchi wa Tanzania katika sehemu kubwa
kutothamini utalii
                               1.Hawajui utalii ni kitu gani?
                               2.Hawajui ni umuhimu wa utalii
                               3.Wanashindwa kumudu gharama kwani gharama za chakula na malazi ni kubwa
                               4.Ugumu wa maisha
                               5.Umbali  hadi kufika sehemu  za utalii.
                               6.Kutothaminiwa kwa watalii wandani na watoa huduma.

Shime Tanzania nchi nzuri yafaa sasa kubadilika na kwenda na mfumo mpya wa maisha kwa kupenda na kuthamini utalii wa ndani kuleta michngo ya nini kifanyike kuleta mabadiliko katika sekta ya utalii ili Tanzania yetu isiwatoe tu ushamba wazungu bali na sisi Wazawa.

Elimu ya utalii inayotolewa mashuleni kuanzia ngazi ya chini IBORESHWE ili iwe ya kumjenga mtanzania atambue umuhimu wa utalii katika maisha yake ya kila siku   katika ngazi zote za  elimu Tanzania.

Pia imefika muda sasa Tanzania kutumia utalii  kutangaza utaifa  kama njia mojawapo ya kutuunganisha na kuwa kitu kimoja kama ilvyokuwa  hapo zamani kwa kuwa na vazi la Taifa
                                                             






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni