![]() |
Shule hizo zipo katika mji wa Mlandizi mkoani humo na vimesababisha
wanafunzi hao kuporomoka kimasomo kwa kuwa wanatumia muda mwingi kukaa
machimbo ya mchanga na vichakani kwa ajili ya kufanya vitendo hivyo.
Katika uchunguzi uliofanywa na NIPASHE imebainika vitendo hivyo
hufanywa nyakati za asubuhi wakati vipindi vya masomo vinaendelea na
jioni mara wanapotoka shuleni.
Kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo, mahudhurio ya wanafunzi
kwenye shule hizo yamekuwa ya kusuasua na kusababisha walimu kuwa na
kazi ya ziada ya kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo.
Uchunguzi huo umefanywa katika shule za msingi za Mtongani, Azimio na Jamhuri zote zipo ndani ya mji huo wa Mlandizi.
JINSI HALI ILIVVO
Katika hali inayoonyesha kuwa ni mbaya kwenye shule hizo, baadhi ya
wanafunzi wameonekana kuathirika kisaokolojia na kupungukiwa na uwezo
wa kimasomo darasani.
Hata hivyo, afya za wanafunzi hao zipo hatarini kutokana na hofu ya
kuambukizwa magonjwa ya zinaa ukiwamo Ukimwi baada ya watu wazima
kuhusishwa kuwaingilia.
Baadhi ya walimu wa shule hizo walipozungumza na gazeti hili
walikiri kuwapo kwa vitendo hivyo na kwamba vimeongezeka kwa kasi ya
kutisha na kuwapa hofu.
Walisema walengwa wa vitendo hivyo ni wanafunzi kuanzia darasa la
tatu hadi la nne ambao mara nyingi wanalazimishwa kulawitiwa na
wanafunzi wenzao wa madarasa ya juu.
Aidha imedaiwa wanafunzi wengine wanafanyiwa vitendo hivyo na watu
wazima wakiwa nyumbani kwao na kwenye mabanda ya kuonyesha picha za
video nyakati za usiku.
"Tatizo hili limekuwa kubwa, walimu tumejitahidi kupambana nalo
kwa kiasi kikubwa lakini inaonyesha hatujafanikiwa," alisema Mwalimu
Jamila Kipengele wa Shule ya Msingi Mtongani.
Mwalimu Kipengele ambaye anaongoza kitengo cha taaluma, alisema
vitendo hivyo vinafanyika katika maeneo hayo ambapo huko wanafunzi
wanakutana mara wanapofanikiwa kutoroka wakati wa vipindi vya masomo.
"Tunavyosikia huko machimbo wanakuwa watoto kutoka shule tofauti na
kutendeana matendo hayo machafu, baada ya kugundua jambo hilo tuliamua
kufanya msako mkali wa kuwakamata wote wanaohusika na kuwarudisha
shuleni," alisema Kipengule.
Kwa shule ya Azimio, Mwalimu Emmanuel Mwambeja ambaye anafundisha
darasa la tatu, alieleza nusu ya wanafunzi 98 wa darasa lake hawaingii
darasani katika vipindi vya jioni na badala yake wanaishia kwenye
machimbo.
Mwalimu Tetula Kessy wa Shule ya Msingi Azimio, ambaye yupo kwenye
kamati ya kuzuia unyanyasaji wa watoto chini ya Plan Tanzania, alisema
wanafunzi wengi wanajikuta wakiingia katika vitendo hivyo kutokana na
kushawishiwa na watu wazima na kuangalia picha za ngono kwenye mabanda
yaliyozunguka kila eneo kwenye shule hizo.
"Tunapokaa na kuwauliza kwa nini wanafanya hivyo, wanajibu kwamba
walikuwa wakifanyiwa nyumbani au wanaona kwenye vibanda vya video na wao
wanajaribu kwa wenzao," alisema Mwalimu Kessy.
WATOTO WASEMA
Katika Shule ya Msingi Jamhuri baadhi wanafunzi wameeleza upo
wakati wanafunzi walifikia hatua ya kupasua kaptula zao upande wa nyuma
ili kurahisisha kuingiliwa na wenzao.
Baadhi ya wanafunzi ambao majina yao yanahifadhiwa, walisema
wanafunzi hao walikuwa na kawaida kwenda kwenye korongo lililo jirani na
shule hiyo na kisha kulawitiana.
"Wanachana kaptula sehemu ya nyuma kwa kutumia wembe, tulikuja
kugundua wanaporudi darasani wanakuwa katika hali tofauti ndipo tukaamua
kuripoti kwa walimu," alisema mwanafunzi mmoja.
Kauli za wanafunzi hao ziliungwa mkono na Mratibu wa Elimu Kata ya
Kilangalanga, Thomas Tito, ambaye alisema amefanya juhudi kubwa
kupambana nalo wakati alipokuwa Mwalimu Mkuu katika shule hiyo.
"Nakumbuka nilipokuwa naongoza shule hiyo niliwakuta wanafunzi
wamepasua kaptula zao kwa nyuma na wembe, nilipodadisi niligundua
wanafanya mchezo huo hatari kwa sababu wanapotoka huko vichakani
wanakuwa wamechafuka sana," alisema.
Kufuatia hali hiyo aliamua kuripoti katika vyombo vya sheria kwa
ajili ya kuchukuliwa hatua lakini ilishindikana baada ya kuonekana
watoto hao walikuwa wakilawitiana wenyewe kwa wenyewe.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni