Jumanne, 18 Machi 2014

WIZI WA KAZI ZA WASANII TANZANIA KIKWAZO UKUAJI TASINIA HII


MSANII WA NYIMBO ZA INJILI WA  WA WIKI


                                                                                                                                                               Karibu  mpenzi msomaji na mfuatiliaji katika ukurasa huu wa mahojiano ya wasanii wa injili wanaotamani kuinuka katika tasinia hii ya muziki wa injili  lakini  kwasababu moja au nyingine au kutokana na changamoto mbalimbali hushindwa kutimiza malengo yao, katika  ukurasa huu tunafanya mahojiano  wasanii wachanga wanaotamani kuinuka na walioonyesha nia ya kweli ya kutamani kujikita katika injili kwa njia ya uimbaji, karibu sana na fuatana na mimi mwanzo hadi mwisho.


Katka ukura6sa huu leo nina mleta kwenu msanii wa nyimbo za injili kutoka katika kanisa la MARANATHA RECONCILIATION CHURCH – MANZESE kwa jina anatambulika  kama PRISCA FRANK MAGOMA anasifu na kuabudisha kan kanisani ambapo timu ya mwangaza media ilimshuhudia akiiendesha huduma hiyo kanisani kwao  na kuamua kumfuatilia kujua mengi kuhusu tasinia hii   timu ya mwangaza media iliamua  kumtembelea  kazini kwake  na kufanya mahojiano nae kuhusu mambo mengi sana katika tasinia hii ya injili (kwa njia ya uimbaji) ambapo hadi hivi sasa  albamu yake ya nyimbo nane  ipo studio kwa ECK PRODUCTION magomeni mwembechai

PICHA ZOTE NI PRISCA .MAGOMA AKIWA KAZINI KWAKE MAGOMENI POPOBAWA BARABARA YA SINZA KUPITIA TANDALE UZURI NDANI YA  ROBIN PHOTO STUDIO& GRAPHICS DESIGN

                                                                                                                                                                                
 
HISTORIA YAKE KWA UFUPI
Kwa jina naitwa PRISCA FRANK MAGOMA , Nimezaliwa Tarehe 09-12-1983  ni mtoto wa pili kati ya watoto sita wa mzee Magoma ni mzaliwa wa mkoa wa KILIMANJARO  wilaya ya SAME.
Elimu yangu ni kidato cha nne katika shule ya sekondari ya MSAKI MEMORIAL ya kibamba jijini Dar es salaam.

Nimeolewa na nina  watoto wawili  tangu mwaka 2006 ambapo kwa muda wote huo nipo katika ndoa kipindi tunaoana na mume wangu alikuwa anafanya kazi ya ualimu katika wilaya  ya KIBAHA  VIJIJINI  kisha baadae tulihamia DAR baada ya mume wangu kuamua kuacha kazi na kuamua kuingia kwenye ujasiriamali.  Ambapo kwa sasa tupo Dar  na kazi yetu ni biashara kama mnavyoniona  hivyo hapa nipo ofisini kwangu. “alisema dada Prisca”

MALENGO YAKE
Kwa ujumla malengo yangu ni mengi ila  ufupi
===Napenda mungu aniinue kiroho na nipende kutenda mapenzi yake siku zote 
=== Niweze  kufanya kazi ya mungu  kwa utimilifu  kupitia nyimbo za injili.
=== kuwa na familia inayompenda mungu na kutenda mapenzi ya mungu
 


KUHUSU ALBAMU YAKE
Albamu ipo studio kwa ECK PRODUCTION magomeni mwembechai inaendelea kutengenezwa siwezi kusema imefikia hatua gani  ila ipo karibu sana kutoka  nategemea kazi itakuwa nzuri sana  wapernzi wa mziki wa injili wategemee kitu kizuri  na mabadiliko makubwa katika tasinia hii ya muziki wa injili.

 



CHANGAMOTO KATKA TASINIA  YA NYIMBO ZA INJILI
Changamoto ni nyingi ila zilizochukua uzito  ni gharama za maandalizi ya albamu studio kiasi kinachotakiwa ni kikubwa  kiasi kwamba  waimbaji wengi hasa wanoibukia wan ashindwa kumudu, pia kwa wengine ipo changamoto ya  rushwa ya mapenzi  kwa waandaaji wa mziki wa injili na wasambazaji wa mziki huu. Zaidi ya zote kwangu mimi ni wizi wa kazi za wasanii unaoendelea katika maeneo mengi ya jiji na hata mikoani  ni vyema wanaofanya wizi huo waache kwani ni dhambi  kufanya hivyo na inamnyima mapato msanii na serikali pia inakosa kodi.


Ahsannte ndugu mpenzi wa kurasa hii ya m,sanii wa wiki kupitia MWANGAZA MEDIA tangu mwanzo wa  mahojiano nakusihi endelea kufuatilia ukurasa huu utapata mengi sana na kwa wale wanaopenda timu ya MWANGAZA MEDIA iwatembelee  waendelee kutembelea ukurasa huu hapo baadae tutatoa fomu maalumu ya maombi.


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni