Jumatatu, 24 Machi 2014

Hotuba ya Jaji Warioba yapongezwa na Wajumbe CCM




Baadhi  ya Wajumbe wa Bunge la katiba kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameipongeza hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.

Hayo yamejitokeza pale mjumbe Seleman Jafo, alisema Jaji Warioba ameibua vitu vingine ambavyo hajawai kuvisikia tangu awe mwanasiasa na kwamba msimamo wake mpaka sasa ni kusimamia ukweli bila kuangalia maslahi ya Chama chake anachotoka. Alisema pia Jaji Warioba ameweka wazi na kufanya mustakabali wa taifa hili unaweza kwenda sehemu ambayo sio nzuri endapo hatua za haraka hazitachukuliwa kuhusiana na suala hilo la Muungano.

Paulo Kimiti alisema kuwa licha ya kuunga mkono hotuba ya Jaji Warioba, lakini vitu alivyoeleza vyote ni vya msingi katika mustakabali wa Taifa.Alisema kwa mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010, kutambua Zanzibar ni nchi huru ndani ya Muungano kunaufanya Muungano kuwa wa nchi mbili na serikali mbili badala ya nchi moja.

Kimiti alisema kinachopaswa kufanywa sasa na wajumbe wa bunge hilo ni kujadili rasimu bila ushabiki wa vyama na makundi.
Innocent Kalogeris, Mbunge Morogoro kusini, CCM alisema taarifa aliyotoa Jaji Warioba inadhihirisha udhaifu wa uongozi kwani tayari katiba imevunjwa, lakini kinachotakiwa ni kufanya marekebisho ya kusaidia kuimarisha Muungano na sio kuanzisha Serikali tatu.

Ezekiel Maige, alisema Rasimu iliyowasilishwa inahitaji kufanyiwa marekebisho makubwa na Bunge hilo kwa kuwa haijaziba mianya ya upotevu wa rasilimali za nchi.Jumuiya  na Taasisi za Kiislam Tanzania, zimeunga mkono hotuba ya Jaji Warioba.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni